Mamlaka ya Habari na TEHAMA ya Kenya na Kampuni ya Teknolojia ya Huawei zimekamilisha mafunzo kwa watumishi wa umma ili kuongeza ujuzi wao kuhusu teknolojia.
Naibu mkuu wa mambo ya umma ya Kampuni ya Huawei nchini Kenya Bibi Fiona Pan, amesema mafunzo hayo yanayotolewa kwa njia ya mtandao wa Internet, yanalenga kuwapa watumishi ujuzi wa sasa kuhusu TEHAMA, Serikali Mtandao, mji unaotumia teknolojia za kisasa, muunganiko kupitia Internet na usalama wa mtandao. Watumishi zaidi ya 400 wa serikali ya Kenya walijiandikisha katika kipindi cha kwanza cha mafunzo hayo ya siku tano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |