Wizara ya mambo ya nje ya Nigeria imesema, itajitahidi kuhakikisha waziri wa zamani wa fedha wa nchi hiyo Bibi Ngozi Okonjo-Iweala anashinda na kuwa mkurugenzi mpya wa Shirika la Biashara Duniani (WTO).
Msemaji wa wizara hiyo Bw. Ferdinand Nwoye amesema, Nigeria itaendelea kushirikiana na wadau wake kuhakikisha kuwa nia ya mgombea wake Bibi Okonjo-Iweala kuongoza WTO inatimia.
Lakini, msemaji wa WTO Bw. Keith Rockwell amesema, ujumbe wa Marekani umetangaza kuendelea kumuunga mkono mgombea kutoka Korea Kusini, Bi. Yoo Myung-hee.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |