Watu tisa wamefariki papo hapo kwenye ajali ya barabarani iliyotokea katika Kaunti ya Kilifi iliyoko pwani nchini Kenya.
Kamanda wa polisi wa tarafa ya Rabai Stephen Matu amesema, majeruhi saba wakiwemo watoto wawili wanapata matibabu katika hospitali ya Kaunti ndogo ya Mariakani, huku wawili kati yao wakiwa na hali mbaya. Pia amesema ajali hiyo ilisababishwa na mwendo wa kasi na uendeshaji mbaya wa gari.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |