Kamati ya Haki za Binadamu ya Ethiopia EHRC imetangaza kuwa, watu zaidi ya 32 wameuawa katika shambulizi la silaha lililotokea katika Jimbo la Oromia nchini Ethiopia. Kamati hiyo imesema kuwa washambuliaji hao walilenga watu wa kabila la Amharas ambalo ni kabila la pili kwa ukubwa nchini humo. Kamati hiyo imezihimiza mamlaka zinazohusika kufanya uchunguzi huru juu ya mauaji hayo na pia kutafuta sababu za jeshi kujiondoa kutoka eneo hilo ambalo linajulikana kuwa na hatari ya kushambuliwa, na kuchukua hatua mwafaka kuhakikisha usalama wa raia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |