Wizara ya mambo ya ndani ya Afghanistan imesema, wapiganaji watatu na watu 19 wameuawa na wengine 22 kujeruhiwa katika shambulizi dhidi ya Chuo Kikuu cha Kabul.
Wizara hiyo imesema, wapiganaji kadhaa wamelipua mabomu na kuvamia chuoni na kupambana na kikosi cha kulinda usalama cha Afghanistan kilichowasili baadaye.
Mpaka sasa, hakuna kundi lolote lililotangaza kuhusika na shambulizi hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |