Serikali ya Burundi imesema kuwa itafungua tena anga yake Jumapili ya tarehe 8 mwezi huu, baada ya kufungwa kwa karibu miezi minane kutokana na hatua za kuzuia kuenea kwa janga la COVID-19.
Taarifa ya msemaji wa serikali ya nchi hiyo, Prosper Ntahorwamiye imesema, wasafiri wote wanaoingia na kutoka nchi hiyo watalazimika kuonesha matokeo ya vipimo vya COVID-19 vilivyofanywa ndani ya saa 72 kabla ya safari zao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |