Inspekta mkuu Doreen Malambo wa Zambia, anayehudumu katika Tume ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), ametunukiwa tuzo ya kuwa Ofisa wa Polisi Mwanamke wa Umoja wa Mataifa wa mwaka huu. Katika hafla ya utoaji wa tuzo iliyofanyika jana Jumanne, msaidizi wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia operesheni za ulinzi wa Amani Jean-Pierre Lacoix amempongeza Malabo kwa kujitolea kwa dhati katika masuala ya usawa wa jinsia, haswa kwa kuhimiza haki za wanawake na wasichana kupitia kuwapa nguvu kudai haki zao na kuimarisha ushiriki wao katika maisha ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |