Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Wang Wenbin amesema, ingawa janga la COVID-19 limeleta athari kwenye mawasiliano ya kimataifa, lakini mwaka huu, wenzi wa "Ukanda Mmoja, Njia Moja" wameanzisha mfumo wa ushirikiano katika nyanja nyingi, na kufanya zaidi ya mikutano 20 ya kimataifa.
Wang amesema ushirikiano wa "Ukanda Mmoja, Njia Moja" unafuata kanuni ya majadiliano, ujenzi wa pamoja na manufaa ya pamoja, na utatoa mchango zaidi wa kuzisaidia pande mbalimbali kukabiliana na janga la COVID-19, kufufua uchumi, na kutimiza Ajenda ya Maendeleo Endelevu ya Mwaka 2030 ya Umoja wa Mataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |