Maonesho ya 3 ya Kimataifa ya Bidhaa Zinazoingizwa China kutoka Nchi za Nje yamefunguliwa leo mjini Shanghai, China. Rais Xi Jinping amehutubia ufunguzi wa maonesho hayo.
Kwenye hotuba yake, rais Xi amesema maonesho hayo yamekuwa jukwaa muhimu la kufanya biashara na mawasiliano ya watu kati ya China na nchi za nje.
Rais Xi amesisitiza kuwa janga la COVID-19 limeleta athari kubwa duniani, jamii ya kimataifa inapaswa kushikamana na kushirikiana zaidi.
Maonesho hayo yatakayofanyika kuanzia tarehe 5 hadi 10 Novemba yameyashirikisha makampuni mbalimbali kutoka nchini China na nchi za nje.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |