Tume ya Uchaguzi nchini Uganda imetangaza kuwa uchaguzi wa rais utafanyika tarehe 14, mwezi Januari mwakani.
Tume hiyo pia imetangaza kuwa wagombea watano kutoka vyama vya siasa akiwemo rais wa sasa wa nchi hiyo Yoweri Museveni na wagombea 6 huru watashiriki kwenye uchaguzi huo.
Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Simon Byabakama ametoa wito kwa wagombea hao kufuata kanuni za kujikinga na COVID-19 na kuhakikisha usalama wa raia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |