Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ametangaza hatua mpya za kupambana na mlipuko wa COVID-19.
Katika hotuba yake kwa njia ya televisheni, Rais Kenyatta amesema, hatua hizo ni pamoja na kupiga marufuku mikutano ya kisiasa kwa siku 60, kuongeza muda wa marufuku ya kutotoka nje wakati wa usiku na kuongeza matumizi ya masomo ya mtandao.
Rais Kenyatta amesema, pamoja na kwamba serikali itaongeza nguvu kupambana na virusi hivyo, lakini nia ya kujikinga ya viongozi na raia ni muhimu zaidi ili kuweza kupata mafanikio.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |