Serikali ya China, kupitia Jumuiya ya Maendeleo ya Wake wa Marais wa nchi za Afrika, imetoa vifaa vya kupambana na COVID-19 kwa wanawake, vijana na watoto katika nchi 53 barani Afrika.
Maofisa wa serikali za nchi Afrika na sekta mbalimbali wamesema, China imesafirisha vifaa hivyo kwa nchi 53 barani humo kwa wakati, na kuwasaidia wanawake, vijana na watoto wa huko kupambana na janga la COVID-19, jambo lililoonesha urafiki mkubwa kati ya wananchi wa pande hizo mbili. Pia wamesema, nchi mbalimbali zinatakiwa kushikilia ushirikiano na mshikamano wa pamoja ili kushinda janga hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |