Idara ya Shirika la Afya Duniani barani Afrika imesema kuwa, janga la COVID-19 limezuia huduma za matibabu ya kimsingi katika Afrika.
Miongoni mwa nchi 13 zilizochunguzwa, kiwango cha huduma ya matibabu kilipungua dhahiri kuliko miaka 2 iliyopita. Habari zinasema, nchi zisizopungua 15 za Afrika ziliahirisha shughuli za kupiga chanjo ya ugonjwa wa surua, homa ya manjano na polio mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |