Jeshi la Nigeria jana lilithibitisha kuwa, majambazi kadhaa wameuawa kwenye shambulizi la anga katika jimbo la Kaduna, Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo. Msemaji wa jeshi la Nigeria Bw. John Enenche amesema, helikopta ya kijeshi ilikuwa imewagundua majambazi hao kwenye msitu wa eneo la Kuzo la jimbo hilo, lakini hakutaja idadi kamili ya majambazi waliouawa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |