• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Timu ya matibabu ya China chafunga safari kuelekea Gambia

    (GMT+08:00) 2020-11-09 20:08:10

    Timu ya wataalamu wa matibabu wa China kimefunga safari kwenda Gambia kuisaidia nchi hiyo kupambana na janga la virusi vya Corona kwa muda wa miezi mitatu.

    Timu hiyo ina wataalam 9 wa magonjwa mahututi, magonjwa ya kuambukiza, magonjwa ya kupumua, uuguzi, usimamizi wa maambukizi hospitali na kinga dhidi ya maambukizi. Wataalam hao watatoa maelekezo kuhusu kinga na udhibiti wa COVID-19 na pia kushiriki kwenye kazi za matibabu nchini Gambia.

    Habari zinasema timu ya nne ya matibabu ya China nchini Gambia itakuwa inafanya kazi za matibabu huko kwa muda wa mwaka mmoja.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako