• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Watu wasiopungua 50 wauawa na wanyamapori nchini Tanzania kila mwaka

    (GMT+08:00) 2020-11-10 09:05:20

    Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA Bw. Mabula Nyanda jana alisema kuwa, watu wasiopungua 50 wanauawa na wanyamapori kila mwaka nchini Tanzania.

    Bw. Nyanda alisema wanyama pori waliotoka kwenye eneo la uhifadhi na kupotea pia wanaharibu hekta 5,000 za mazao ya kilimo kila mwaka. Alibainisha kuwa idadi ya watu wanaouawa na wanyamapori inaongezeka na inapaswa kuchukuliwa hatua za haraka ili kushughulikia hali hii ya kutisha. Kamishna huyo amesema TAWA imeshaandaa mpango unaolenga kudhibiti migogoro ya watu na wanyamapori ambayo inaathiri vibaya binadamu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako