Wizara ya ulinzi ya Russia jana ilithibitisha kuwa, helikopta moja ya MIG-24 ya Russia ilipigwa kombora na kuanguka mpakani mwa Armenia na Azerbaijan, na kusababisha vifo vya wafanyakazi wawili wa helikopta hiyo na mwegine mmoja kujeruhiwa. Wizara ya mambo ya nje ya Azerbaijan imekiri kuwa helikopta hiyo ilishambuliwa kimakosa na jeshi la Azerbaijan, na kuiomba msamaha Russia juu ya ajali hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |