Uchaguzi wa jaji wa mahakama ya kimataifa umefanyika leo. Mgombea kutoka China Bibi Xue Hanqin ambaye pia ni naibu mkuu wa mahakama hiyo, amechaguliwa tena kuwa jaji mpya.
Bibi Xue alichaguliwa kuwa jaji wa mahakama hiyo tangu mwezi Juni, mwaka 2010. Kuanzia mwezi wa Februari mwaka 2018, amekuwa naibu mkuu wa mahakama hiyo, akiwa ni jaji wa kwanza wa kike kutoka China na naibu mkuu wa kwanza wa kike wa mahakama ya kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |