Ingawa timu ya Ghana ilishiriki kwa mara ya kwanza kwenye michuano ya Kombe la dunia mwaka 2006, kwenye michuano hiyo timu ya Ghana iliingia katika nafasi 16 za mwisho. Na kwenye michuano ya Kombe la dunia ya mwaka 2010, timu ya Ghana ilipata hatua ya robo fainali. Kutokana na mafanikio hayo, Ghana si timu ya kupuuzwa.
Wachezaji
Timu ya Ghana ni mpja ya timu zenye viungo wazuri. Licha ya Michael Essien wa klabu ya AC Milan, timu hiyo pia ina Sulley Muntari, Kevin-Prince Boateng. Vilevile ina wachezaji wengine hodari akiwemo Asamoah Gyan, ambaye alicheza vizuri kwenye michuano ya Kombe la dunia ya mwaka 2010.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |