• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China inataka uwazi katika kutekeleza miradi za Ukanda mmoja, Njia moja

    (GMT+08:00) 2019-04-28 10:15:48

    NA VICTOR ONYANGO

    BEIJING, CHINA

    Rais wa China Xi Jinping na viongozi wengine wa ulimwengu wameimisha maana ya kukuza maendeleo ya kiuchumi kwa nchini zote duniani kwa kile bwana Xi alichosema kama kujenga jingo la jumuiya iliyo na baadaye kwa kwa watu kote ulimwenguni.

    Akihutubia viongozi mbali mbali wakati wa ufunguzi rasmi wa kongamano ya Ukanda mmoja, Njia Moja siku ya Ijumaa mjini Beijing, rais Xi alisisitiza haja ya maendeleo sawa katika kushinikiza kuchangia malengo ya maendeleo ya Umoja wa Mataifa ya 2030.

    Rais Xi alisema kuwa tangu mwanzo wa Ukanda mmoja, Njia moja mwaka wa 2013, China imekuwa ikifanya kazi na nchi za wanachama ili kuongeza uunganisho kwa njia ya barabara.

    "Ukanda mmoja, Njia moja imeona miradi mikubwa ya ushirikiano inayopatikana na imeunda fursa nyingi za biashara, na hivyo kuchangia ukuaji wa uchumi duniani na kusaidia China kujifungua kwa dunia kwa mnajili wa biashara," alisema rais Xi, ambaye alikuja na wazo la Ukanda mmoja, Njia moja.

    Rais wa China alitoa wito kwa uwazi katika kutekeleza miradi ya Ukanda mmoja, Njia moja (BRI), akiongezea kuwa China haiwezi kuvumilia rushwa kutolewa wakati wa utekelezaji wa miradi hizo.

    "China itasaidia tu kushirikiana wazi na utawala safi wakati wa kutafuta ushirikiano wa BRI. Tutahitajiki kushirikiana na nchi wachama juu ya jinsi ya kupambana na ufisadi na utawala mzuri kwa kuhusisha vyama vya kisiasa tofauti vya nchi hizo," aelezea bwana Xi.

    Alisisitizia nchi wanachama umuhimu wa kukuza maendeleo ya kijani ili kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa duniani kote.

    Rais Xi aliahidi kuwa China itaendelea kufungua soko lake kwa nchi za kigeni na kutambua kuwa sheria ya uwekezaji wa kigeni itatekelezwa kikamilifu. Aliongeza kuwa serikali yake italinda mali miliki kwa makampuni ya kigeni.

    Kwa upande wake, rais wa Kenya aliyezugumza baadaye, alimsifu mwenzake wa China rais Xi kwa kuahidi kuwa China itafungua soko lake kwa nchi za kigeni. Bwana Kenyatta alisema Kenya itaendelea kutumia fursa kama hizo na kutekeleza Ukanda mmoja, Njia moja Afrikana.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako