• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Afrika Kusini yatarajia kuvutia wawekezaji wachina kupitia CIIE

    (GMT+08:00) 2019-11-11 09:45:00

    NA VICTOR ONYANGO

    SHANGHAI, CHINA

    Naibu waziri wa Biashara na Viwanda wa Afrika Kusini Bi Gina Nomalungelo ameisifu China kwa kujitolea kwake kuendelea kufungua soko lake kubwa kwa ulimwengu.

    Akihutubia waandishi wa habari nje ya banda la nchi hiyo kwenye Maonyesho ya Pili ya Kimataifa ya Uigizaji wa Bidhaa kutoka nje ya China (CIIE) mjini Shanghai mnamo Alhamisi, Bibi Nomalungelo alisema kuwa maonyesho hayo yanayoandaliwa na China kila mwaka yamechangia sana kwa kuwepo na biashara wa kufaidi pande zote.

    "Ukiangalia mwenendo wa biashara kati yetu na China, tunasaidiana sana, pia tuna majukwaa mengine, ambayo yatafungua zaidi linapokuja suala la uagizaji wa bidhaa na usafirishaji. Ukiangalia jinsi tunavyofanya biashara na China, ilikuwa ndogo sana. Kwa hivyo sasa, tuko hapa na bidhaa, pia time kwa tukiongeza thamani kwa bidhaa zetu," alisema.

    Alisema kuwa Afrika Kusini inashiriki kwa mara ya pili tangu kuanzishwa kwa CIIE mwaka jana na kampuni za nchi hiyo ziko Shanghai kupata ushirikiano zaidi na wenyeji wa China na kampuni mbalimbali za kichina.

    "Tunatumahi kuwa maonyesho haya yakifungwa Jumapili, kampuni ambazo ziko hapa kuonyesha bidhaa zao, watapata mawasiliano na miunganisho na watafungua fursa zaidi za biashara na hivyo basi, uhusiano wetu na China utaendelea kunawiri kwa kiwango cha juu," asema waziri Nomalungelo.

    Aliongeza kuwa maonyesho hayo sio muhimu kwa Afrika Kusini pekee bali nchi zingine za Afrika kuwaambia ulimwengu na China kwamba kuna bidhaa bora zaidi katika bara.

    Bibi Nomalungelo alizitaka pia mataifa ya Afrika kutochukua fursa hiyo lakini kuja na bidhaa zenye ubora na idadi akibainisha kuwa duo hilo limezuia biashara kati ya China na bara kwa muda mrefu.

    Alifichua kuwa nchi hiyo iko tayari kupanua wigo wa biashara yake kupitia ushirika wa vitendo kama maonyesho hayo.

    Kauli yake inaambatana na ile ya Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta katika maonyesho ya Shanghai ya 2018, alipouliza China kufungua soko lake zaidi na kusaidia nchi za Afrika kufikia usafi unayotakikana wakati usafirishaji.

    Lakini akizungumza wakati wa ufunguzi wa CIIE ya pili, Rais wa China Xi Jinping alisema kuwa maonyesho hayo yanasaidia kwenye kuongeza ufikiaji wa bidhaa za nje katika soko la China kwani nchi inafanya juhudi za kupunguza kutofautisha kwa biashara kuu na washirika wake.

    Maonyesho hayo yatamalizika siku ya Jumapili na ilivutia zaidi ya kampuni 3000 kutoka nchi 150 na mashirika ulimwenguni.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako