8: Elimu, Sayansi na Teknolojia

Wanafunzi wa Ng'ambo Nchini China

Katika miaka ya hivi karibuni, uchumi wa China unaongezeka kwa haraka, na hadhi ya China duniani inainuka siku hadi siku, na kuwavutia vijana wengi zaidi wa nchi za nje kuja kusoma nchini China. Hivi sasa, wanafunzi elfu 77 kutoka nchi mbalimbali duniani wanasoma nchini China, ambapo asilimia 90 kati yao wanafunzi wanajilipia wenyewe. Wanafunzi hao wanatoka nchi na sehemu zaidi ya 170 kama vile Korea ya Kusini, Japan, Marekani, Vietnam, Indonesia, Thailand, Ujerumani, Russia, Nepal, Ufaransa, Australia na Malaysia.

Kozi ambazo wanafunzi wa ng'ambo wanaosomea ni Kichina, utamaduni wa China, historia ya China, na utibabu wa Kichina. Katika miaka ya hivi karibuni baadhi ya wanafunzi pia wameanza kusomea kozi za sheria, mambo ya fedha na uchumi, uhasibu na kozi nyingine za kisayansi.

China inachukua hatua mbalimbali za kuongeza wanafunzi wa ng'ambo, kwa mfano kuwaruhusu wanafunzi wa ng'ambo kuishi nje ya shule ili waweze kuingiliana na wakazi wa China, na kufahamu zaidi mambo ya China; kutoa mihadhara kwa lugha za Kichina na Kiingereza kwa wanafunzi wa shahada ya pili, ili kuwavutia wanafunzi wasiojua sana lugha ya Kichina.

Kutokana na takwimu zisizokamilika, tangu kuasisiwa kwa China mpya hadi leo, idadi ya wanafunzi wa ng'ambo waliosoma nchini China imezidi laki 6 na elfu 30 kutoka nchi na sehemu 170 duniani. Wanafunzi hao wanatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi zao, na kuhimiza maingiliano na ushirikiano kati ya nchi zao na China.

Kujifunza Kichina

Kujifunza Kichina ni lengo la wanafunzi wengi la kuja China kwa mafunzo. Hivi sasa asilimia 60 ya wanafunzi wa ng'ambo nchini China wanajifunza Kichina. Kipindi cha kujifunza Kichina hakina muda maalum, kuna darasa la kipindi cha miezi kadhaa au wiki kadhaa, pia kuna elimu ya Kichina ya shahada ya kwanza ya miaka minne. China imetunga vitabu vya aina mbalimbali vya kiada kwa ajili ya wanafunzi wa ng'ambo, walimu wanatoa mafunzo kwa lugha mbili za Kichina na Kiingereza au kwa Kichina pekee kutokana na kiwango tofauti cha wanafunzi.

Hivi sasa vyuo vikuu zaidi ya 300 vya China vinaweza kupokea na kufundisha wanafunzi wa ng'ambo Kichina, wanafunzi wanaotaka kusoma nchini China wanaweza kuwasiliana moja kwa moja na vyuo hivyo.

Kuanzia mwaka 1992, China ilianzisha mtihani wa kiwango cha lugha ya Kichina unaofanana na TOEFL kwenye lugha ya Kiingereza. Hivi sasa China imeweka vituo vya mtihani wa aina hiyo katika nchi na sehemu 28 duniani.

Kusoma Katika Chuo Kikuu Nchini China

Wanafunzi wakitaka kusoma katika vyuo vikuu nchini China wanatakiwa kuwa na shahada husika na kiwango fulani cha lugha ya Kichina, baadhi ya vyuo vikuu pia vitawapa mtihani maalum kabla ya kuwaandikisha. Wanafunzi wa nchi za nje wanaweza kuwasiliana na vyuo vikuu vya China kwa kupitia mtandao, wakiandikishwa, watarahisishwa urasmu wa kuja China. Hivi sasa vyuo vikuu zaidi ya 300 nchini China vinawaandikisha wanafunzi wa nchi za nje.

Gharama za shule nchini China ni za chini, na inatofautiana kati ya vyuo tofauti, hivi sasa karo ya mwaka mmoja ni kiasi cha yuan elfu 20 kwa wastani.

China inazingatia sana kupata wanafunzi wa ng'ambo kusomea elimu ya juu , na kulifanya jambo hilo kama njia muhimu ya kuinua hadhi yake ya kimataifa katika eneo la elimu, na kuvifanya vyuo vikuu viwe vya daraja la kwanza duniani. China itaendelea kuchukua hatua za kuboresha mazingira, ili kuwavutia wanafunzi wengi zaidi wa ng'ambo, hasa wanafunzi wa shahada ya pili.


1 2 3 4 5 6 7