• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (3 Juni-9 Juni)

    (GMT+08:00) 2017-06-09 19:13:25

    Watu 10,000 wakimbia moto pwani ya Afrika Kusini

    Watu takriban 10,000 wamelazimika kukimbia makwao kutoka mji mmoja pwani ya Afrika Kusini ambao umeharibiwa pakubwa na moto.

    Wanajeshi wanashiriki katika juhudi za kukabiliana na mtaa huo kukabili moto huo ambao unawaka katika maeneo 25 katika mji wa Knysna.

    Watu wanane wamefariki kutokana na upepo mkubwa na moto ambao umekumba mji huo na maeneo mengine katika kanda ya Cape Magharibi.

    Upepo huo mkubwa umesaidia kueneza moto huo.

    Nyumba zaidi ya 150 zimeteketezwa eneo hilo kwa mujibu wa shirika la wazimamoto.

    Mji huo una takriban wakazi 77,000.

    Unapatikana kilomita 500 mashariki mwa mji wa Cape Town.

    Wanajeshi karibu 150 watatumwa eneo hilo kuzuia wahalifu kupora mali katika maeneo ambayo wenyewe wamekimbia.

    Mwezi Mei, mkoa wa Cape Magharibi ulitangaza janga ya ukame baada ya mabwawa mawili makubwa kukauka kabisa.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako