• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (29 Julai-4 Agosti)

    (GMT+08:00) 2017-08-04 20:16:50

    Mvutano wa kisiasa waendelea kushuhudiwa DRC

    Serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo kupitia Waziri wa Mambo ya Ndani na Usalama, Basile Olongo, imesema kuwa hali ya usalama ni tulivu katika miji kadhaa iliyoshuhudia makabilianao makali kati ya jeshi la polisi na waandamanaji, siku ya Jumatatu katika nchi hiyo.

    Bw Olongo amesema maandamano yaliyoandaliwa na vuguvugu la vijana linalopigania mabadiliko, demokrasia na uongozi bora LUCHA yalikuwa yamepigwa marufuku na serikali.

    Wanaharakati hawa wanasema maandamano yao yalikuwa yenye lengo la kushinikiza kufanyika kwa uchaguzi mwaka huu, lakini pia kupinga uongozi wa rais Joseph Kabila.

    Kwa upande wa vyama vinavyomuunga mkono rais Joseph Kabila vimesema hakuna haja ya kuharakisha uchaguzi huo.

    Kwa ujumla waandishi wa habari 13 Walikamatwa nchini humo, huku wakipokonywa vifaa vyao vya kazi, lakini baada ya saa mbili waliachiwa huru.

    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako