• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (9 Septemba-15 Septemba)

    (GMT+08:00) 2017-09-15 17:46:36

    Urusi na Belarus zaanza mazoezi ya pamoja ya kijeshi,

    Urusi na Belarus zimeanza mazoezi makubwa ya pamoja ya kijeshi, ambayo yamepewa jina Zapad-2017, na ambayo yamezitia wasiwasi nchi jirani wanachama wa shirika la kujihami la nchi za Magharibi la Nato.

    Mazoezi hayo ni moja ya mazoezi makubwa kabisa ya kijeshi kuwahi kufanywa na Urusi tangu ilipotwaa rasi ya Crimea kutoka kwa Ukraine mwaka 2014.

    Wizara ya ulinzi ya Urusi imesema wanajeshi 12,700 wanashiriki, lakini wataalamu wa Nato wanatarajia kwamba idadi itakuwa juu zaidi ya hiyo.

    Mazoezi hayo ya kijeshi yanafanyika ndani na maeneo ya karibu na belarus na yanashirikisha vifaru, ndege za kivita na manowari.

    Rais wa Ukraine Petro Poroshenko ameonya kuwa Zapad-2017 (jina ambalo maana yake kwa Kirusi ni "Magharibi") huenda ikawa ni hatua ya mwisho kabla ya kuivamia Ukraine.

    Kiev imeimarisha ulinzi wake mpakani.

    Makundi ya wapiganaji wanaoungwa mkono na Urusi wanadhibiti maeneo makubwa ya mashariki mwa Ukraine na wameendelea kukabiliana na wanajeshi wa serikali.

    Hii ni licha ya kutiwa saini kwa makubaliano ya kusitisha mapigano Februari mwaka 2015 mjini Minsk.

    Nato imeituhumu Urusi kwa kuwapa waasi hao silaha kalikali pamoja na wanajeshi.

    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako