• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (March 17-March 23)

    (GMT+08:00) 2018-03-23 17:44:45

    Rais Mnangagwa awaachia huru wafungwa 3000

    Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa ambaye alichukua madaraka hayo toka kwa mtangulizi wake Robert Mugabe mwezo Novemba mwaka jana, amewaachia huru wafungwa zaidi ya 3000 kwa lengo la kupunguza idadi ya wafungwa ambao wamefurika kwenye magereza ya nchi hiyo.

    Msamaha huu wa rais utashuhudia kuachiwa kwa wafungwa wote wa kikem walemavu na watoto huku waliohukumiwa kifungo cha maisha jela msamaha huu ukiwa hauwahusu.

    Wafungwa wanaoumwa na wale ambao wamezidi umri wa miaka 60 na ambao wametumikia robo tatu ya kifungo chao pia wataachiwa huru.

    Taarifa hiyo imesema kuwa jumla ya wafungwa 3000 wataachiwa huru na kufanya idadi ya wafungwa waliobakia kufikia elfu 17.

    Imeongeza kuwa wafungwa ambao wanasubiri kunyongwa na ambao wameshatumikia kifungo cha miaka 10 jela hawatanyongwa tena na badala yake watatumikia kifungo cha maisha jela.

    Nchi hiyo ilitekeleza adhabu ya kunyonga mara ya mwisho ilikuwa mwaka 2005 na rais Mnangagwa ni mmoja wa watu walio mstari wa mbele kupinga adhabu ya kifo.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako