Mtoto wa rais wa zamani wa Angola aanza mgomo wa kula
Mtoto wa rais wa zamani wa Angola, José Eduardo dos Santos, ambaye anazuiliwa jela tangu Jumatatu wiki hii mjini Luanda katika kesi ya ubadhirifu, ameanza mgomo wa kula, vyanzo kutoka jela vimesema.
Mkurugenzi wa zamani wa Mfuko wa kitaifa wa Angola, Jose-Filomeno dos Santos mwenye umri wa miaka 40 anazuiliwa katika jela la Sao Paulo kwa agizo la ofisi kuu mashitaka.
Jose-Filomeno dos Santos anayefahamika kwa jina la Zenu, alishtakiwa mnamo mwezi Machi mwaka huu kwa madai ya "ufisadi, kujitajirisha kinyume cha sheria, kushirikiana na wahalifu" na kuweza kupitisha mlango wa nyuma akiwa pamoja na washirika wake hadi dola biloni 1.5.
Ni wa kwanza kutoka familia ya rais wa zamani dos Santos kufungwa tangu mrithi wake Joao Lourenço kuchukuwa hatamu ya uongozi wa nchi mwaka mmoja uliopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |