• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Septemba 22-Septemba 29)

    (GMT+08:00) 2018-09-28 19:10:36

    Mtoto wa rais wa zamani wa Angola aanza mgomo wa kula

    Mtoto wa rais wa zamani wa Angola, José Eduardo dos Santos, ambaye anazuiliwa jela tangu Jumatatu wiki hii mjini Luanda katika kesi ya ubadhirifu, ameanza mgomo wa kula, vyanzo kutoka jela vimesema.

    Mkurugenzi wa zamani wa Mfuko wa kitaifa wa Angola, Jose-Filomeno dos Santos mwenye umri wa miaka 40 anazuiliwa katika jela la Sao Paulo kwa agizo la ofisi kuu mashitaka.

    Jose-Filomeno dos Santos anayefahamika kwa jina la Zenu, alishtakiwa mnamo mwezi Machi mwaka huu kwa madai ya "ufisadi, kujitajirisha kinyume cha sheria, kushirikiana na wahalifu" na kuweza kupitisha mlango wa nyuma akiwa pamoja na washirika wake hadi dola biloni 1.5.

    Ni wa kwanza kutoka familia ya rais wa zamani dos Santos kufungwa tangu mrithi wake Joao Lourenço kuchukuwa hatamu ya uongozi wa nchi mwaka mmoja uliopita.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako