• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Januari 12-January 19)

    (GMT+08:00) 2019-01-18 16:35:08

    Fatou Bensouda akata rufaa dhidi ya uamuzi wa kuachiliwa kwa Laurent Gbagbo

    Rais wa zamani wa Cote d'Ivoire Laurent Gbagbo na waziri wake wa zamani Charles Ble Goude huenda wakaendelea kusalia kwa muda mrefu kuliko ilivyotarajiwa katika jela la Scheveningen.

    Jumatano jioni Mwendesha mashitaka wa ICC Fatou Bensouda alikata rufaa dhidi ya uamuzi wa kuachiliwa huru siku moja baada ya ICC kumfutia mashataka Gbagbo na msaidizi wake Charles Ble Goude na kuamuru waachiliwe huru.

    Mwendesha mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa (ICC), Fatou Bensouda, ameomba Laurent Gbagbo na Charles Ble Goude kuendelea kuzuiliwa jela, wakati anaendelea kupata na kutathmini sababu zilizopelekea majaji kuamua kuachiliwa huru.

    Fatou Bensouda ana hofu kwamba rais wa zamani wa Cote d'Ivoire na waziri wake wa zamani wanaweza kutoroka kabla ya kuendelea kwa kesi dhidi yao.

    Kwa upande mwingine, ikiwa majaji watano watakataa rufaa na kuthibitisha uamuzi wa mahakama wa kuwafutia mashitaka, hatua itakayofauata ni kuachiliwa huru bila masharti.

    Tayari nchi ya Ubelgiji imekubali kumpokea Laurent Gbagbo kama ataachiliwa huru.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako