• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Novemba 9-Novemba 15)

    (GMT+08:00) 2019-11-15 20:19:23

    Bunge la Tanzania lapitisha sheria ya mtu kujipima VVU mwenyewe

    Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Leo Novemba 12, 2019 limepitisha Sheria inayotoa mamlaka kwa mtu kujipima Virusi vya UKIMWI mwenyewe.

    Sheria hiyo, Itaruhusu mtu yeyote kuanzia miaka 15 na kuendelea kujipima mwenyewe jambo ambalo awali lilikuwa linafanyika kwenye vituo vya afya pekee.

    Akiongea mapema baada ya bunge kupitisha sheria hiyo, Naibu Waziri wa Afya, Mhe. Faustine Ndugulile amesema Sheria hiyo itasadia watu wengi hususani wenye uoga kujipima kwa urahisi.

    Ndugulile amesema kuwa kwa sasa kundi linaloongoza kwa maambukizi mapya ya VVU ni vijana ambapo wasichana ndio wanaoongoza kwa asilimia kubwa huku wanaume wakitajwa kuwa kundi linaloongoza kuogopa kupima virusi vya UKIMWI.


    1  2  3  4  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako