• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Desemba 7-Desemba 13)

    (GMT+08:00) 2019-12-13 20:26:14
    TZ: Mfungwa mmoja baada ya kupata msamaha wa Rais, alifanya tukio la wizi na kurejeshwa tena gerezani.

    Ni kweli sikio la kufa haliskii dawa. Siku mbili tu baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli, kutoa msamaha kwa wafungwa 70 mkoani Njombe, mmoja wa wafungwa hao Musa Msolwa, amekamatwa na Jeshi la Polisi, kwa kuvunja na kuiba kwenye nyumba ya wageni Mjini Makambako. Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Khamis Issah, amesema mfungwa huyo amedumu nje ya msamaha kwa saa nane tu baada ya hapo akaenda kufanya tukio la uhalifu kwa kuvunja, moja ya nyumba za wageni mkoani Njombe.

    Akizungumza baada ya kutiwa nguvuni na Jeshi la Polisi, Msolwa amesema kuwa aliingiwa na shetani licha ya kuwa aliahidi kubadilika, lakini ameshindwa.


    1  2  3  4  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako