12: Wanawake

Maingiliano ya Kimataifa

Hali ya Jumla ya Maingiliano Kati ya Wanawake wa China na wa Nchi za Nje

Tokea mwezi Juni mwaka 1995 Shirikisho Kuu la Wanawake la China likiwa jumuiya ya kwanza isiyo la kiserikali ya China kupata hadhi ya kushiriki katika mikutano ya Umoja wa Mataifa, limeshiriki kwa juhudi katika shughuli za Umoja wa Mataifa na za pande nyingi za kimataifa, limetuma wajumbe kuhudhuria mikutano mingi ya Umoja wa Mataifa, kama vile mkutano wa kamati ya haki za binadamu, mkutano wa kamati ya hadhi ya wanawake, mkutano maalum wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu suala la wanawake na la watoto, na mkutano wa wakuu wa dunia kuhusu suala la maendeleo endelevu. Shirikisho Kuu la Wanawake la China limetoa sauti na mchango katika kulinda amani ya dunia na maslahi ya nchi zinazoendelea na maendeleo ya harakati za wanawake duniani.

Mashirikisho ya wanawake ya China yamefanya maingiliano na ushirikiano na nchi za nje kwa njia mbalimbali. Hivi sasa Shirikisho Kuu la Wanawake la China limeanzisha uhusiano wa kirafiki na mashirikisho 700 ya wanawake na watoto ya nchi 151, kujishirikisha mambo ya wanawake ya Umoja wa Mataifa na ya pande nyingi, lilifaulu kuandalia mkutano wa 4 wa wanawake wa dunia na mkutano wa kubadilishana maarifa wa mkutano huo, kongamano la wanawake kati ya China na Umoja wa Ulaya na mkutano wa viongozi wanawake wa Shirika la Ushirikiano wa Uchumi la Asia na Pasifiki APEC. Mashirika ya wanawake ya China pia yamefanya ushirikiano wa kimataifa ili kuwahudumia vizuri wanawake na watoto wa China, yamekuwa mashirika ya wanawake yanayojulikana duniani.

Miradi ya Wanawake ya Ushirikiano wa Kimataifa

Kutokana na kuimarishwa kwa maingiliano kati ya wanawake wa China na wa nchi za nje, mashirika mengi zaidi na zaidi ya wanawake wa China yameanza kutumia miradi ya ushirikiano ya kimataifa na nadharia ya kimaendeleo ya kimataifa kutatua masuala halisi ya wanawake wa China. Katika miaka 5 iliyopita, Shirikisho Kuu la Wanawake la China limefanya miradi ya ushirikiano na mashirika mengi ya kimataifa, kutoa mchango mkubwa katika kuboresha mazingira ya kuishi na kujiendeleza kwa wanawake na watoto wa China kwa kuboresha afya ya wanawake, kutokomeza hali ya kutojua kusoma wala kuandika na kutoa mikopo mdogo. Shirikisho Kuu la Wanawake la China limesifiwa sana na mashirika ya kimataifa kwa ufanisi mkubwa na uaminifu.

Katika miaka ya hivi karibuni, mashirika ya wanawake ya China yameanzisha miradi mingi ya ushirikiano na jumuiya husika za wanawake za kimataifa, mashirikisho hayo ni pamoja na: "Mradi wa sheria ya wanawake kati ya China na Canada" (mwaka 1998). Huu ni mradi wa ushirikiano unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa ya Canada na kutekelezwa kwa pamoja na Shirikisho Kuu la Wanawake la China na Chuo Kikuu cha Mitaa cha Canada. Mradi huo unalenga kutekeleza vizuri zaidi sheria na taratibu husika kuhusu haki na maslahi ya wanawake, na kulinda haki za wanawake kwa kuinua mwamko na uwezo wao wa kutumia sheria, kuinua mwamko wa kijinsia wa wanasheria na uwezo wa mashirika ya wanawake wa kueneza sheria na kuwaelimisha wanawake. Wanawake wengi wa sehemu inayotekeleza mradi huo wameanza kujua jinsi ya kulinda haki na maslahi yao kwa kutumia sheria.

Miradi mingine ya ushirikiano kati ya jumuiya za wanawake wa China na ya kimataifa ni kama vile "mradi wa kupinga na kuzuia uuzaji wa wanawake na watoto wa sehemu ya delta ya mto Mekong" na "mradi wa kuwasaidia wanawake waliopunguzwa kazini kupata ajira mpya".

Shirikisho Kuu la Wanawake la China pia limefanya ushirikiano na Shirika linaloshughulikia Mambo ya Watoto la Umoja wa mataifa UNICEF, idara ya maendeleo ya kimataifa ya Uingereza na mashirika mengine kuhusu watoto wa kike. Miradi hiyo inalenga kubadili mitizamo na mienendo mibaya ya watu ya kuwabagua watoto wa kike, kuwasaidia watoto wa kike wawe na uwezo wa kujishirikisha katika maendeleo ya uchumi na jamii na kujua jinsi ya kulinda haki na maslahi yao.

Tokea mwaka 1999, miradi ya ushirikiano wa kimataifa imesaidia kujenga shule nyingi za msingi au madarasa kwa ajili watoto wa kike ili kuwawezesha watoto wa kike wa China waliolazimika kuacha shule kutokana na matatizo ya kiuchumi warudi shuleni.


1 2 3 4 5 6 7