• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Januari 21-Januari27)

    (GMT+08:00) 2017-01-27 18:40:14

    Rais Adama Barawa awasili Gambia kutoka Senegal baada ya kuapishwa rasmi

    Bw. Adama Barrow ameregea nchini Gambia baada ya kuapishwa kuwa rais wa nchi hiyo kwenye ubalozi wa nchi hiyo mjini Dakar, Senegal.

    Bw. Barrow alichaguliwa kuwa rais kwenye uchaguzi uliofanyika tarehe 2 Desemba mwaka jana, lakini hawezi kuchukua madaraka moja kwa moja kutokana na upinzani wa rais wa zamani Yahya Jammah.

    Umoja wa Ulaya uliingilia kati na kumshurutisha aliekuwa rais Jammeh aheshimu matokeo ya uchaguzi na kukabidhi madaraka kwa Bw. Barrow.

    Mjumbe wa Umoja wa Mataifa katika kanda ya Afrika magharibi Bw. Mohamed Ibn Chambas ameliarifu Baraza la usalama la umoja huo kuwa Umoja wa Mataifa umeunga mkono utulivu na ujenzi wa Gambia.

    Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric amesema, rais Adama Barrow wa Gambia aliyeapishwa katika ubalozi wa nchi hiyo nchini Senegal ameregea Gambia wiki hii.


    1 2 3 4 5 6 7
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako