• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (11 Machi-17 Machi)

    (GMT+08:00) 2017-03-17 18:36:53

    Maafisa 2 wa Umoja wa Mataifa watekwa nyara DRC

    Maafisa wawili wa Umoja wa Mataifa wametekwa nyara katika jimbo la Kasai ya Kati, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, chanzo cha usalama katika umoja wa mataifa kimebaini

    Mateka hao ni Michael Sharp kutoka Marekani na Zaida Kikatalani, raia wa Sweden.

    Kwa mujibu wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, watu hao pamoja na raia wanne wa DRC (waendesha pikipiki za kukodiwa na mkalimani wao) walitekwa nyara na kupelekwa katika msitu.

    Vurugu baina ya vikosi vya usalama na wanamgambo zimeendelea kuukumba mkoa wa Kasai ya Kati tangu mwezi Septemba 2016.

    Makabiliano hayo tayari yameingia katika mkoa jirani wa Kasai Mashariki na Lomani.

    Karibu watu mia nne wameuawa katika machafuko hayo yanayoendelea katika maeneo hayo.


    1 2 3 4 5 6 7 8
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako