• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (15 Aprili-21 Aprili)

    (GMT+08:00) 2017-04-21 19:21:05

    Waziri mkuu wa Uingereza atangaza kufanya uchaguzi mkuu mapema kuliko ilivyopangwa

    Waziri mkuu wa Uingereza Bi. Theresa May amesema Uingereza itafanya uchaguzi mkuu tarehe 8 mwezi Juni mwaka huu, ikiwa ni mapema kabla ya ilivyopangwa awali, ili kutoa urahisi kwa serikali yake kufanya mazungumzo na Umoja wa Ulaya kuhusu kuanza mchakato wa kujitoa kwenye Umoja huo.

    Bi. May amesema, lengo la uamuzi huo ni kulinda vizuri zaidi maslahi ya Uingereza.

    Tarehe 29 mwezi uliopita, Bi. May alitangaza kuzindua rasmi utaratibu wa Uingereza kujitoa kwenye Umoja wa Ulaya, na mara utaratibu huo ukianza rasmi, Uingereza italazimika kukamilisha mazungumzo ndani ya miaka miwili.

    Kutokana na sheria ya Uingereza, muda wa serikali ya awamu hiyo kuwa madarakani utamalizika mwaka 2020, hata hivyo kufanya uchaguzi mkuu mapema bado kunahitaji kupitishwa na bunge la Uingereza.


    1 2 3 4 5 6 7 8 9
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako