Watu wanne wauawa kwenye mapigano baada ya waasi wa Houthi kudhibiti msikiti mkubwa nchini Yemen
Wafuasi wanne wa aliyekuwa rais wa Yemen Bw. Ali Abdullah Saleh wameuawa kwenye mapigano yaliyotokea jana kati yao na waasi wa kundi la Houthi mjini Sanaa.
Taarifa iliyotolewa na chama cha GPC cha Bw. Saleh, inasema wafuasi wake wengine sita pia walijeruhiwa kwenye mapigano hayo, baada ya waasi wa Houthi kutwaa msikiti mkubwa uliojengwa na kupewa jina la Saleh.
Mapigano hayo yaliibuka kufuatia wafuasi wa Saleh kuwazuia maelfu ya wafuasi wa Houthi kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa mtume Mohammad katikati ya mji wa Sanaa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |