• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Aprili 7-Aprili 13)

    (GMT+08:00) 2018-04-13 15:40:28

    Nchi za Ulaya kuwafukuza wanadiplomasia zaidi wa Urusi

    Jumuiya ya nchi za Kujihami za Magharibi NATO juma hili imeungana na mataifa mengine 25 duniani kuwafurusha wanadipolomasia wa Urusi katika kile kinachoonekana ni kujibu kile wanachosema ni hatua ya Serikali ya Moscow kutumia sumu inayoathiri mishipa ya fahamu dhidi ya jasusi wake wa zamani jijini London.

    Hatua hii imeelezwana nchi ya Uingereza kama ukurasa mpya wa namna mataifa ya magharibi yatashirikiana na Urusi.

    NATO imewafukuza wanadiplomasia 7 wa Urusi na kukataa kutoa vibali kwa wengine watatu na kufanya idadi ya watu wanaotajwa kuwa wapelelezo wa Urusi waliofukuzwa kufikia 150 wakiwemo wale 23 waliofukuzwa na Uingereza.

    Katika kile kinachoonekana sio kitu cha kawaida, nchi 25 zimeungana na Uingereza kuchukua hatua kutokana na tukio la Machi 4 ambapo jasusi wa zamani wa Urusi Sergei Skripal na mwanae wa kike Julia waliwekewa sumu kwenye mji wa Salisbury.

    Serikali ya London na washirika wake wanailaumu Serikali ya Moscow kwa kile wanachosema utawala huo kutumia sumu ya Novichok ambayo inadaiwa kutumiwa na Urusi kushambulia raia wake waliokimbia.

    Waziri wa mambo ya kigeni wa Uingereza Boris Johnson amesema kufukuzwa kwa wanadiplomasia hao ni pigo kwa Urusi ambayo itachukua muda mrefu kujenga idara yake ya ujasusi.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako