DRC yatangaza kumalizika kwa mlipuko wa Ebola
Waziri wa afya wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC Bw. Oly Ilunga ametangaza rasmi kumalizika kwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.
Bw. Ilunga ameshukuru kasi na ufanisi wa utekelezaji wa hatua zilizochukuliwa na serikali na wadau wake katika kutoa chanjo kwa watu 3,300 ili kukabiliana na ugonjwa huo.
Baada ya kuidhinishwa na serikali ya DRC, timu ya Shirika la afya duniani WHO na madaktari wasio na mipaka MSF walitoa chanjo kwa watu 3,330 nchini humo.
Wizara ya afya ya DRC imetangaza kuwa, tangu Ebola ilipoibuka nchini DRC tarehe 8 Mei, watu zaidi ya 54 wamefariki wakiwemo 14 waliothibitishwa kuambukizwa Ebola.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |