Uganda, Rwanda, Burundi na Sudani kusini zimetakiwa kuchukua tahadhari kuhusu ebola
Shirika la afya duniani WHO limesema kuwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola nchini humo bado hauhitaji jitihada za dharura za kimataifa huku likisisitiza kuwa linaufuatilia kwa karibu sana ugonjwa huo.
Kauli hii inakuja baada ya mkutano maalumu wa dharura uliofanyika mjini Geneva kujadili hali ya ugonjwa huu nchini DRC.
Kauli ya mwisho iliyokubalika katika kikao hicho ni kwamba hatua zinahitaji kushinikizwa katika kupambana na ugonjwa huo hatari.
Uganda, Rwanda, Burundi na Sudani kusini zimetakiwa kuchukua tahadhari ya haraka kutokana na kusambaa kwa ugonjwa huu, kwasababu hali inaweza kubadilika wakati wowote kuanzia sasa.
Kumeshuhudiwa ongezeko la visa vya Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na mzozo unaoendelea, Kupoteza imani kwa jamii katika maeneo yalioathirika, yote haya yanatatiza jitihada za kudhibiti ugonjwa huo.
Mapigano katika eneo hilo yanafanya kuwa vigumu kudhibiti ugonjwa huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |