• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Oktoba 13-Oktoba 19)

    (GMT+08:00) 2018-10-19 19:43:20

    Tume ya Ukweli Haki na Maridhiano yaanzishwa Gambia

    Gambia imezindua Tume ya Ukweli Haki na Maridhiano, kuchunguza visa vya ukiukwaji wa haki za binadamu vilivyotokea wakati wa rais wa zamani Yahya Jammeh.

    Tume hiyo hiyo itakuwa na Makamishena 11 ambao tayari wameapishwa jijini Banjul kuanza kazi hiyo.

    Kuanzia mwisho wa mwezi Oktoba, watu mbalimbali walioteswa au kunyanyaswa wanatarajiwa kwenda kutoa ushahidi wao mbele ya Tume hiyo.

    Shirika la Kimataifa la kutetea haki za Binadamu la Human Rights Watch limesema raia wa nchi hiyo walioteswa, kubakwa wakiwa jela au kulazimishwa kunywa dawa zilizotengezwa na Jammeh ili kuponya maambukizi ya Ukimwi watajitokeza kutoa shuhuda zao.

    Rais Adama Barrow amesema kuwa, Tume hiyo itasaidia sana katika uponyaji wa nchi hiyo.

    Tume hii kama ilivyokuwa ile ya Afrika Kusini, itasikiliza shuhuda dhidi ya watu mbalimbali kipindi chote cha miaka 22 alichoongoza Jammeh ambaye amepewa hifadhi nchini Equitorial Guinea.


    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako