• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Novemba 17-Novemba 23)

    (GMT+08:00) 2018-11-23 19:02:22

    Raia wa Italia atekwa Pwani ya Kenya

    Watu wenye silaha wamemteka raia wa Italia, katika kijiji cha Chakama, katika kaunti ya Kilifi Pwani ya Kenya.

    Ripoti zinasema kuwa, watu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Al Shabab ndio waliohusika.

    Imebainika kuwa raia huyo wa kigeni, mwenye umri wa miaka 23 ambaye pia mfanyikazi wa kujitolea na watu wengine watano, walijeruhiwa katika makabiliano yaliyoshuhudiwa.

    Polisi wanasema mtoto mwenye umri wa miaka 10, ni miongoni mwa watu hao waliojeruhiwa. Imeelezwa kuwa, mtoto huyo alipigwa risasi machoni na anaendelea kupata matibabu hospitalini.

    Utekaji nyara nchini Kenya sio jambo la kawaida, lakini linapotokea, limekuwa likisababisha madhara kwa sekta ya utalii nchini humo.

    Mwaka 2011, raia wa Uingereza aliuawa kwa kupigwa risasi na mkewe akatekwa huku Mwanamke mmoja raia wa Ufaransa akitekwa na watu wenye silaha nyumbani kwake katika kisiwa cha Lamu.

    Aidha, wafanyikazi wawili wa Shirika la kutoa msaada kutoka nchini Uhispania pia walitekwa.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako