• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Aprili 6-Aprili 12)

    (GMT+08:00) 2019-04-12 19:08:22

    Magavana wa Kabila watwaa ushindi mkubwa

    Chama cha Kabila cha PPRD na washirika wake wanaojumuika katika muungao wa kisiasa wa FCC wameshinda kwa mara nyingine uchaguzi wa Magavana na Manaibu Gavana, uchaguzi ambao ulifanyika Jumatano Aprili 10, 2019 katika mikoa 22 kati ya 26 inayounda DRC.

    Chama cha UDPS cha rais Felix Tshisekedi kimepata Gavana mmoja pekee katika mkoa wa Kasai Oriental, pamoja na muungano wa vyama vya upinzani wa Lamuka.

    Katika mikoa minne (Haut-Lomami, Kasaï ya Kati, Nord-Ubangui na Tshopo), duru ya pili ya uchaguzi itafanyika Jumamosi wiki hii.

    Uchaguzi huu ni pigo kubwa kwa rais wa sasa wa DRC Felix Tshisekedi, ambaye muungano wake wa CASH una viti vichache katika baraza la Wawakilishi, Bunge la Seneti na katika Baraza la Wawakilishi katika ngazi za mikoa.

    Kwa hiyo Felix Tshisekedi atalazimika kuunda serikali yenye Magavana wengi kutoka kambi ya mtangulizi wake.

    Ndugu ya aliyekuwa rais wa DRC Joseph Kabila, Zoe Kabila, ambaye sasa ni gavana wa Tanganyika, ni miongoni mwa waliochaguliwa.

    Naye Christophe Nangaa, ndugu wa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (CENI) Corneille Nangaa, amechaguliwa kuwa Gavana wa mkoa wa Haut-Uélé dhidi ya mgombea wa FCC.


    1  2  3  4  5  6  7  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako