• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Mei 9-Mei 15)

    (GMT+08:00) 2020-05-15 20:33:10

    MAFURIKO: 237 wafa huku 800,000 wakiachwa bila makao

    WAZIRI wa Ugatuzi Eugene Wamalwa amefichua kuwa kufikia Jumatano asubuhi jumla ya watu 237 walikuwa wamefariki maeneo mbalimbali nchini kutokana na mafuriko.

    Aliongeza kuwa zaidi ya familia 161,000 (sawa na jumla ya watu 800,000 ) zimeachwa bila makao huku mali ya thamani isiyojulikana ikiharibika.

    Alisema huenda idadi hiyo ikapanda kwa sababu mvua ya masika inatarajiwa kuendelea hadi mwishoni mwa mwezi huu wa Mei.

    Alisema hayo Jumatano kwenye kikao na wanahabari Nairobi baada ya kuzuru kaunti za Nakuru na Narok kukagua hasara iliyosababishwa na janga hilo.

    Maeneo yaliyoathirika zaidi ni karibu na Ziwa Victoria, Ziwa Naivasha, Mto Tana, Mto Nzoia na Kati mwa Kenya karibu na mito ambayo huelekeza maji katika Mto Tana kutoka milima ya Aberdares.


    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako