• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Mei 16-Mei 22)

    (GMT+08:00) 2020-05-22 21:13:03

    Kenya yasema kilele cha ugonjwa wa COVID-19 ni katika miezi ya Agosti na Septemba

    Kenya imewatahadharisha raia wake kuwa kilele cha ugonjwa wa Covid 19 kitakuwa miezi ya Agosti hadi Septemba ambapo watakuwa wakirekodi waathirika karibia 200 kwa siku. Mkurugenzi wa Afya ya Umma Patrick Amoth, amesema maambukizi yameingia katika ngazi ya kijamii ambayo ni hatari zaidi.

    Janga la corona bado linajidhihirisha kuwa changamoto katika mataifa mengi duniani. Kenya nayo haijaachwa. Katika siku za hivi karibuni, Kenya imekuwa ikirekodi waathiriwa wengi zaidi waliopata maambukizi ikilinganishwa na awali.

    Hivi sasa Kenya inapanga kuanza kupima watu zaidi ya 3,000 kwa siku kuanzia hivi karibuni. Hilo linajitokeza wakati ambapo wizara ya afya imedokeza kuwa na vifaa vya kutosha vya kupima virusi vya corona ambavyo vinaweza kudumu hata kwa mwezi mzima.


    1  2  3  4  5  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako