• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Septemba 19-Septemba 25)

    (GMT+08:00) 2020-09-25 16:14:40

    Huenda Shule Zifunguliwe Oktoba 19

    SHULE huenda zikafunguliwa Oktoba 19, iwapo serikali itakubali mapendekezo ya kamati inayosimamia masuala ya elimu nchini katika kipindi hiki cha kukabili virusi vya ugonjwa wa Covid-19.

    Kulingana na ripoti ya kamati hiyo, wanafunzi wa Darasa la Nane na wale wa Kidato cha Nne watafanya mitihani yao ya kitaifa ya KCPE na KCSE mtawalia mwezi wa Aprili mwaka ujao.

    Kamati hiyo imependekeza pia kalenda ya shule za msingi na upili kubadilishwa ili muhula wa kwanza uwe ukianza Juni.Hapo kesho, Waziri wa Elimu, Prof George Magoha, anatarajiwa kuipokea ripoti hiyo ya kamati.

    Inatarajiwa baadaye wadau watashauriana na Rais Uhuru Kenyatta ambaye ataidhinisha uamuzi wa mwisho utakaotolewa.

    Kwenye mapendekezo yake ya kwanza, kamati hiyo inataka wanafunzi wa Darasa la Saba na Nane, Kidato cha tatu na cha Nne warudi shuleni Jumatatu, Oktoba 19.Wanafunzi wa Darasa la Nne, ambao ndio wa kwanza kutumia mtaala mpya wa masomo, wanatarajiwa kuripoti shuleni siku hiyo pia.

    Kwenye mapendekezo ya pili, kamati hiyo imependekeza wanafunzi wote kuripoti shuleni siku moja, Oktoba 19.

    Serikali imetenga Sh1.9 bilioni kutengeneza madawati ya shule za msingi na zile za sekondari.Prof Magoha aliwaelekeza wakurugenzi wa elimu wa maeneo na kaunti kuhakikisha madawati hayo yamefika shuleni ifikapo Oktoba 19.

    Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Wakuu wa Shule za Upili (Kesha), Bw Kahi Indimuli alisema wako tayari kufungua na kuwaomba wadau wengine kujitokeza na kusaidia shule kujiandaa.

    Katibu mkuu wa muungano wa waalimu za sekondari (Kuppet), Bw Akelo Misori pia alisema wakati umefika wa shule kujiandaa kufunguliwa.


    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako