• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Oktoba 31-Novemba 6)

    (GMT+08:00) 2020-11-06 16:54:56
    Viongozi wakuu nchini Kenya watakiwa kufanya mazungumzo kuhusu BBI

    Rais Uhuru Kenyatta, naibu wake William Ruto, Kinara wa ODM, Raila Odinga na viongozi wa vyama vingine vikuu nchini Kenya wameshauriwa kushiriki mazungumzo kutafuta mwafaka kuhusiana na utata unaozingira Mpango wa Upatanishi BBI.

    Wazee wa Jamii za Kenya wanadai kuwa hapana haja ya viongozi kuwa na misimamo tofauti kuhusu BBI, hali ambayo ikalazimu kura ya maoni kufanyika nchini.

    Wameongeza kuwa iwapo kura ya maoni itaandaliwa huenda ikachochea uhasama miongoni mwa jamii mbali mbali na kusababisha machafuko.

    Aidha wamesisitiza kuwa fedha ambazo zinapendekezwa kuandaa kura ya maoni ni nyingi na zinaweza kutumika kuwasaidia wakenya ambao wanapitia hali ngumu ya maisha.


    1  2  3  4  5  6  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako