• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii (Novemba 7-Novemba 13)

    (GMT+08:00) 2020-11-12 20:35:19
    China kuipa kipaumbele Afrika katika utoaji wa chanjo ya covid-19

    Serikali ya China imeapa kuipa Kenya, watu wake na Afrika kwa ujumla kipaumbele pindi tu itakapopata chanjo ya ugonjwa wa COVID-19. Balozi wa China nchini Kenya Bwana Zhou Pingjian alibainisha kuwa utawala wa Rais Xi Jinping utaendelea kusimama na nchi zinazoendelea, hasa barani Afrika, katika juhudi zinazolenga kushinda janga hilo ambalo limesababisha mateso kwa binadamu pamoja na mgogoro mkubwa zaidi wa kiuchumi na kijamii.

    Akizungumza baada ya mkutano na kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga, Zhou alisisitiza ahadi ya nchi yake "kuchukua uongozi katika kutafuta chanjo salama na yenye ufanisi katika kutibu COVID-19 na kuitoa kwa bei nafuu pamoja na kuhakikisha inapatikana kote Afrika", ofa iliyokaribishwa na kiongozi huyo wa Chama cha Orange Democratic Movement.

    "Tunataka kuishukuru serikali ya China kwa ahadi yake ya kuhakikisha kuwa pindi chanjo itakapokuwa tayari, itapatikana kwa urahisi na kwa bei nafuu barani Afrika," Raila alisema.

    Tayari chanjo ya COVID-19 iliyotengenezwa na kampuni ya China National Biotech Group (CNBG) iko katika hatua za mwisho za majaribio katika nchi kadhaa ikiwa ni pamoja na baadhi ya mataifa barani Afrika ikiwemo Morroco.

    Watafiti wameonyesha imani yao katika chanjo hiyo ambayo wanasema ni salama kwani tayari imeidhinishwa katika mpango wa dharura nchini China inayowalenga wafanyakazi muhimu na wengine walio katika hatari kubwa ya maambukizi.

    Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani WHO, kati ya chanjo kumi za virusi vya corona ambazo zimeendelea hadi kufikia majaribio ya awamu ya tatu duniani, nne zinatengenezwa na wanasayansi wa China.


    1  2  3  4  5  6  7  8  
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako