China yarusha satelaiti mpya ya uchunguzi wa dunia
2020-12-28 09:10:36| CRI

China yarusha satelaiti mpya ya uchunguzi wa dunia_fororder_1126913930_16090875298611n

China imefanikiwa kurusha satelaiti mpya ya uchunguzi wa dunia kutoka kituo cha kurushia satelaiti cha Jiuquan, kaskazini magharibi mwa China jana usiku.

Satelaiti hiyo ya Yaogan-33 iliyorushwa kwa kutumia roketi ya Long March-4C, imeingia kwenye obiti kama ilivyopangwa, na itatumika kwenye majaribio ya kisayansi, uchunguzi wa raslimali za ardhi, makadirio ya uzalishaji wa kilimo na pia kuzuia maafa.