TZ: Serikali kutumia Ndege kudhibiti nzige Longido
2021-02-23 15:32:56| cri

 

Serikali imewatoa hofu wananchi wa maeneo ya Longido na kuwataka wasiwe na hofu kufuatia nzige walioovamia wilayani humo wakitokea nchi jirani ya Kenya.

Hayo yamebainishwa na jana Februari 21, na Waziri wa Kilimo, Prof. Adolf Mkenda, baada ya kutembelea eneo la Longido ambalo limevamiwa na nzige  na kuwa kuanzia leo ndege maalum itafanya kazi kupulizia viuatilifu kuua nzige hao.

Prof. Mkenda amesema wananchi wasiwe na hofu nzige wote watadhibitiwa kupitia wataalam wa Wizara ya Kilimo waliopo kwenye maeneo yote yenye dalili za uwepo wa wadudu hao.

Prof. Mkenda amesema nzige wa jangwani wana athari kubwa katika uzalishaji wa mazao ya chakula  na malisho ya mifugo na kundi moja la nzige lina uwezo wa kuruka  bila kutua kwa umbali wa  kilometa 150 Kwa siku.

Aidha, nzige wana uwezo wa kula Sawa na uzito wake  kwa siku ambapo kundi moja la nzige linaweza kuwa na wastani wa nzige milioni 40 kwenye eneo la kilometa  moja za mraba alisema Waziri Mkenda .