Wastani wa pato la taifa kwa mtu nchini China wazidi dola elfu 10 za kimarekani kwa miaka miwili mfululizo
2021-03-01 09:32:26| CRI

Wastani wa pato la taifa kwa mtu nchini China wazidi dola elfu 10 za kimarekani kwa miaka miwili mfululizo_fororder_1127150605_16145196184091n

Takwimu zilizotolewa na Idara Kuu ya Takwimu ya China zinakadiria kuwa, mwaka jana wastani wa pato la taifa kwa mtu nchini China ulifika yuan elfu 72,447, sawa na dola za kimarekani karibu elfu 11.2, ambalo ni ongezeko la asilimia 2 ikilinganishwa na mwaka 2019.

Naibu mkuu wa Idara Kuu ya Takwimu ya China Bw. Sheng Laiyun amesema, mwaka 2020 Pato la Ndani (GDP) la China lilizidi yuan trilioni 100, sawa na dola za kimarekani karibu trilioni 15.45, na pato la taifa kwa mtu mmoja mmoja lilizidi dola elfu kumi za kimarekani kwa miaka miwili mfululizo, na uchumi wa China ulichukua zaidi ya asilimia 17 ya uchumi wa dunia katika mwaka 2020.

Wastani wa pato la taifa kwa mtu nchini China wazidi dola elfu 10 za kimarekani kwa miaka miwili mfululizo_fororder_1127150605_16145196182681n

Takwimu hizo pia zinaonesha kuwa, mwaka jana China iliandikisha kampuni mpya zaidi ya milioni 25, na hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huo, idadi ya kampuni nchini China ilifikia milioni 140.

Wastani wa pato la taifa kwa mtu nchini China wazidi dola elfu 10 za kimarekani kwa miaka miwili mfululizo_fororder_1127150605_16145196184431n