Sudan yasisitiza kubadilisha njia ya mazungumzo kuhusu Bwawa la GERD
2021-04-06 09:14:21| cri

 

 

Sudan imesisitiza kubadilisha njia ya mazungumzo kuhusu Bwawa la Grand Rianissance Rianissance (GERD) baada ya siku 200 “zisizo na ufanisi”. Waziri wa mambo ya nje wa Sudan Bibi Mariam Al-Mahdi amesema duru za mazungumzo yaliyofanyika chini ya usimamizi wa Umoja wa Afrika hazikuwa na ufanisi, na kusababisha kurudi nyuma kwa matokeo yaliyofikiwa katika mazungumzo ya awali.